Watafiti wamefanya utafiti na kugundua kuwa kuna aina tatu ya jinsi ambavyo mwanadamu (watoto) huweza kujifunza mambo.
1. Kujifunza Kwa Njia ya Kuhusianisha Mambo (Classical conditioning)
Kujifunza kwa kuhusianisha mambo kujilikanako kama (classical
Conditioning) ni aina ya kujifunza ambapo mtoto anajifunza jambo kwa
kuhusianisha na kitu fulani.
Kwa mfano kama unasafiri na kila
ukisafiri unaporudi unarudi na zawadi kwa mtoto basi mtoto atahusianisha
safari na zawadi kwamba ukiona baba au mama amesafiri basi ujue
anaporudi lazima atakuja na zawadi.
Mgunduzi wa aina hii ya
kujifunza kwa njia ya kuhusianisha (Classical Conditioning - Learning
Through Association) Bwana Pavlov alifanya utafiti kwa kutumia mbwa.
Kila mara alipokuwa anataka kumpa chakula alianza kwa kugonga kengere
kwanza na mbwa akazoea kwamba ukisikia mlio wa kengere ujue chakula
kimekuja.
Kuna wakati alikuwa anakwenda na kengere bila chakula,
lakini mbwa mara zote aliposikia mlio wa kengere alikuwa akitarajia
kupata chakula kwasababu alikuwa akiusianisha kengere na chakula.
2. Kujifunza kwa Njia ya Pongezi au Zawadi (Oparent Conditioning -Learning through Rewards)
Njia ya pili ya kujifunza mambo inaitwa kujifunza kwa njia ya pongezi
au zawadi yaani (Oparent Conditioning - Learning through Rewards)
iligunduliwa na mtafiti Edward L. Thondike na B.F Skiner.
Katika njia hii mtoto anapata kujifunza kwa kupitia kuwepo au kuondolewa kwa pongezi na zawadi.
Kuna aina mbili za mtoto kujifunza kwa njia ya ongezi au zawadi.
• Kupokea pongezi na zawadi anapofanya vizuri (Positive reinforcements)
Hii humaanisha kwamba mtoto anapokuwa amefanya jambo zuri anapokea
pongezi au zawadi fulani kupitia pongezi au zawadi hizo mtoto anajifunza
kwamba endapo atafanya jambo zuri basi anatarajio la kupokea pongezi au
zawadi.
Mfano wa Baba yangu aliniahidi kuwa nikifanya vizuri kimasomo na nikajua kingereza atanipeleka nairobi kuishi huko
Wakati huo nairobi ilikuwa inaonekana kama Marekani ya Watanzania.
• Kupoteza Nafasi ya Kupokea pongezi na zawadi anapofanya vibaya (Negative reinforcements)
Hii humaanisha kwamba mtoto anapokuwa amefanya jambo baya au hajafanya
kile alichokuwa anatarajiwa kukifanya, basi ile pongezi au zawadi ambayo
ilikuwa aipate kwa sasabu ya kutokufanya vizuri basi ile zawadi au
pongezi inaondolewa anakuwa haipati tena.
Hiyo inamfundisha kwamba kumbe kama akifanya kinyume ana anachotarajiwa kukufanya basi atakosa zawadi au pongezi fulani fulani.
Mfano wa Kijana wangu
Kuna mwaka sikumfanyia Birthday maana akikosea adhabu yake ikawa mwaka
huu hakuna birthday party alimumia sana kwa kukosa sherehe hizo.
3. Kujifunza Kwajia ya Kuchunguza au Kutazama Bila Mhusika Kujua. (Observational Learning)
Aina hii ya tatu ya kujifunza kwanjia ya kuchunguza au kutazama bila
mhusika kujua, iligunduliwa na mtafiti Albert Bandura ambaye aligundua
kwamba, mtu anaweza kujifunza mambo yanayo fanyika kwa kuangalia tu
mifano na tabia za watu wengine wanapokuwa wakifanya jambo.
Watoto walioona wazazi wao wakihusiana usiku na walipokuwa wakicheza
kasichana na kavulana wakavua nguo wakaanza kuona yale waliyo yaona
yakitendwa na wazazi wao.
Most is Caught than Taught
Kulingana na mtafiti Albert Bandora, kujifunza kwa kuchunguza kuna husisha hatua nne muhimu:
• Kuweka Umakini - Attention
Kuweka umakini kwa mtu au kwa tabia zake anavyofanya.
• Kukumbuka kile kilichofanywa na yule mtu mhusika - Retention
Anayejifunza lazima akumbuke kile alichokiona na kujifunza.
• Kufanya kile alichokiona kikifanywa na mhusika - Reproduction
• Motisha - Motivation
Watu wanatabia ya kupenda kuigiza kitu ambacho kinamfurahisha kuliko kile ambacho hakimfurahishi
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO 0784 477775 au Whatup 0784 477775
AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com